Mbiu ya KTN 12 Machi 2016 - Kibunguchi ataka KNEC Ivunjiliwe mbali
12th March, 2016
Kufuatia taarifa kuwa wizi wa mitihani ya KCSE wa mwaka jana ulifanyika, mbunge wa Likuyani Enoch Kibunguchi ametoa wito wa kuvunjiliwa mbali kwa baraza la mitihani la kitaifa knec. Kibunguchi alilalama kwamba matokeo mabaya ya shule eneo bunge lake yalichangiwa na ukosefu wa wizi. Sasa ametishia kuongoza mchakato wa kuwaondoa maafisa wa KNEC waliohusika kwa wizi huo. Waziri wa elimu Fred Matiang’i alikiri kwamba wizi wa mitihani uliongezeka kwa asili mia 70 kwenye mtihani wa kcse mwaka 2015