KTN Leo Kamilifu Machi 11 2016 - Mkurupuko wa kipindupindu
11th March, 2016
Watu 30 wamelazwa hospitali huku ripoti zikiashiria huenda sita wamefariki kutokana na mkurupuko wa kipindupindu maeneo ya Kaunti Za Meru na Tharaka Nithi. Kwa mujibu wa afisa mkuu wa afya kaunti ndogo ya tharaka kaskazini, mkurupuko huo ulianza wakati wagonjwa waliporipoti visa vya kuharisha na sampuli zilipopelekwa kwenye maabara ya kemri, zikabainishwa kuwa ni maradhi ya kipindupindu. Mapema mwezi wa Januari ugonjwa huo uliripotiwa maeneo hayo kabala ya visa vya hivi punde kutokea.