Afya mbovu kisiwani chawatia shaka wakaazi wa Mageta
11th March, 2016
Katika bajeti ya Kaunti Ya Siaya ya kipindi cha mwaka 2015/2016, shilingi bilioni 1.6 zilielekezwa kwa idara ya afya. Lakini katika hospitali ya kisiwa cha mageta taswira ni ya upweke na taabu kwani hospitali hiyo haina dawa, wahudumu wa kutosha na vifaa vingine muhimu licha ya eneo hilo kuwa na idadi ya juu zaidi ya uambukizaji virusi vya HIV ikiwa ni aslimia 23.7 nyuma ya Homabay inayoongoza nchini na asilimia 25.7.