Dkt Karanja Kibicho awaonya machifu wawili kuhusu pombe haramu
10th March, 2016
Baada ya kuwaachisha kazi machifu saba katika kaunti ya Meru hapo jana,katibu katika wizara ya masuala ya ndani mwa nchi leo amefika Nyeri na kuibua wasiwasi mwingi miongoni mwa machifu. Dkt Karanja Kibicho amewasili kuendeleza vita dhidi ya pombe haramu ambapo ameongoza oparesheni ya kumwaga pombe katika maeneo mbali mbali. Machifu wawili walipewa onyo kali mbele ya raia waliofika kuhudhuria mkutano wa hadhara katika eneo la witemere.