Wanawake Embu wamkashifu gavana Wambora kwa kumdhalimu mbunge Cecily Mbarire
8th March, 2016
Ulimwengu mzima ukiadhimisha siku ya wanawake, baadhi ya wanawake katika kaunti ya Embu wamemkashifu gavana wa kaunti hiyo Martin Wambora kwa kutoa matamshi wanayosema yalimkosea heshima mbunge wa Runyenjes Cecily Mbarire. Haya yanajiri huku mada kuu ya siku ya wanawake mwaka huu ikiwa ni kuhakikisha usawa wa jinsia.