Mtoto wa miaka 4 anusurika kifo baada ya kuhusika katika ajali iliyowaua watu 7 papo hapo Salgaa
8th March, 2016
Mtoto wa kike wa umri wa miaka 4 alinusurika kifo kwa tundu la sindano baada ya kuhusika katika ajali ya barabarani iliyowaua watu saba papo hapo katika kivuko cha Ngata Salgaa Nakuru. Mtoto huyo ambaye anatatizika kuzungumza tangu ajali hiyo amelazwa katika hospitali moja mjini Nakuru akiuliza maswali kuhusu walipo wazazi wake.