Wanasiasa wanaswa wakiwahonga wapiga kura Malindi
7th March, 2016
Uchaguzi mdogo katika eneo bunge la Malindi kaunti ya Kilifi umetatizwa kwa madai ya wanasiasa kuwahonga wapiga kura na hitilafu nyenginezo. Mbunge wa Mwea Peter Gitau mapema alikamatwa baada ya kuhusishwa na ununuzi wa wapiga kura. Aidha mbunge wa Kabete Ferdinand Waititu amehusishwa kwenye madai ya kutatiza uchaguzi wa Malindi.