Rais Mastaafu Moi ahimiza serikali izingatie kuboresha elimu ya shule za msingi
6th March, 2016
Rais mstaafu Daniel Toroitich arap Moi ametoa wito kwa serikali kuhakikisha kuwa elimu katika kiwango cha shule za msingi imeboreshwa kwa kiasi kikubwa. Akizungumza kwenye hafla ya kuwatuza wanafunzi katika shule ya upili ya Moi Kabarak, Mzee Moi pia aliwataka wabunge kuzingatia elimu kupitia pesa za ustawi za maeneo bunge. Aliipongeza shule ya upili ya moi kwa kupata matokeo mazuri katika matokeo ya mtihani wa kitaifa wa KCSE 2015