Punda 16 wapatikana wamechinjwa katika kijiji cha Kiambogo mji wa Longonot
29th February, 2016
Takriban punda 16 wamepatikana wamechinjwa katika kijiji cha Kiambogo, karibu na mji wa Longonot. Kisa hicho kimevutia mshangao mkubwa miongoni mwa wenyeji ambao wanahofia kuwa huenda wameuziwa nyama ya punda hao wanaoaminika kuchinjwa usiku wa kuamkia leo.