Uwiano nchini Kenya Miaka 8 baada ya machafuko ya 2008
27th February, 2016
Miaka minane iliyopita wakati sawa na huu taifa la Kenya lilikuwa katika hali mbaya. Jamii za kenya zilikuwa zimegawanyika kwa makabila yenye chuki yakiongozwa na roho wa mauaji na dhuluma. Ilikuwa imesalia siku moja kwa mazungumzo yaliyoongozwa na aliyekuwa katibu mkuu wa umoja wa mataifa Koffi Annan kupata ufanisi. Baada ya mkataba wa maelewano kuafikiwa siku iliyofuata suala moja liliibuka; haja ya kukabili chuki za kikabila ili kupata utangamano. Kwenye awamu ya kwanza ya kisengere-nyuma cha mwaka 2008 Mashirima Kapombe anaangazia suala hilo la uwiano nchini kenya