IEBC: Walemavu wachache wamejitokeza kujisaliji
27th February, 2016
Usajili wa watu wanaoishi na ulemavu katika Kaunti Ya Narok umekumbwa na changamoto hasa kwa kuwa vituo vya usajili vimekuwa vikihamishwa siku baada ya siku. Kufikia sasa idadi ya walemavu waliojisajili ni ndogo. Mwenyekiti wa baraza la walemavu David Ole Sankok ametoa wito kwa IEBC kutafuta njia mbadala za kuwasajili walemavu.