Maendeleo Transnzoia: Umaskini ni wa viwango vya juu
26th February, 2016
Viwango vya umaskini katika kaunti ya Trans-Nzoia vinagonga asilimia 50 ya idadi huku asilimia 60 ya vijana wakiwa hawana kazi. kulingana na Gavana Patrick Khaemba, hali hii imelemaza harakati za maendeleo katika kaunti hiyo inayotambulika kote nchini kwa ukulima. Khaemba alikuwa akizungumza hapa jijini Nairobi katika mkutano na wanahabari na wanabiashara kuhusu kongamano la uwekezaji litakalofanyika katika kaunti hiyo kati ya tarehe 16 hadi 18 mwezi ujao.