Seneta wa Pokot John Lonyangapuo amtaka Duale kujiuzulu
25th February, 2016
Viongozi wa kisiasa wamezidi kutoa kauli mbalimbali kuhusiana na sakata ya NYS ambayo inamkabili aliyekuwa waziri wa ugatuzi Anne Waiguru. Mbunge wa Gatundu kusini Moses Kuria amemuonya Waiguru dhidi ya kuwahusisha wanasiasa katika suala hilo. Naye seneta wa pokot magharibi John Lonyangapuo amemtaka kiongozi wa wengi Adan Duale kujiuzulu baada ya kutajwa na Waiguru.