Mradi wa NYS Kibera ulikuwa njama ya wizi wa mamilioni ya pesa, afichua shahidi kwenye sakata hiyo
23rd February, 2016
Huku mmoja wa washukiwa wa wizi wa fedha katika NYS akihojiwa leo na tume ya kupambana na ufisadi, habari fiche zimeendelea kuibuka kwenye sakata ya wizi wa fedha katika mpango wa NYS. Kikosi cha upekuzi cha KTN kimepata kauli za mwanamke mmoja aliyekuwa akifanya kazi katika idara ya usambazaji ya NYS. Mtumishi huyo anasema mradi wa NYS Kibera ulikuwa ni njama ya wizi wa mamilioni ya pesa