Gor Mahia wacharazwa na CNAPS kutoka Madagascar katika mkondo wa kwanza wa CAF
13th February, 2016
Mabingwa wa ligi kuu ya kandanda nchini gor mahia wameduwazwa kwa kufungwa mabao mawili kwa moja na CNAPS kutoka Madagascar katika mechi ya mkondo wa kwanza ya kinyang’anyiro cha klabu bingwa barani afrika. Kogalo hivi sasa wana kibarua kigumu kufuzu kwa raundi ya pili kwani itabidi wapate ushindi wa mabao mawili au zaidi katika mechi ya mkondo wa pili itakayogaragazwa ugenini tarehe 27 mwezi huu.