Watu saba wafariki kwenye ajali huko Mairiakani kaunti ya Mombasa
13th February, 2016
Watu saba wamepoteza maisha yao hii leo baada ya matatu waliyokuwa wakisafiria kuhusika katika ajali eneo la bonje mariakani kwenye barabara kuu ya Mombasa kuelekea nairobi.matatu hiyo iliyokuwa ikitoka Mombasa kuelekea Voi, iligongana ana kwa ana na lori. Watu watano walifariki papo hapo huku wengine wawili wakifariki pindi tu walipofikishwa katika hospitali ya mariakani. Wanne kati ya waliofariki ni wanawake na watatu ni wanaume. Inaaminika kuwa lori husika lilipoteza mwelekeo wakati ambapo magari hayo yaligongana. Kaimu OCPD wa eneo la kaloleni Patrick Ngeiywa amesema kuwa uchunguzi umeanzishwa kubaini chanzo kamili cha ajali hiyo. Eneo hilo la bonje limetajwa na maafisa wa usalama kama hatari zaidi na waendeshaji magari wametakiwa kuwa waangalifu wanapotumia sehemu hiyo ya barabara. Watu watatu waliojeruhiwa wanaendelea kupata matibabu katika hospitali ya mariakani.