Mshindi wa kwanza wa mchezo wa bahati nasibu- Betway, atuzwa
11th February, 2016
Rodrique Koech ndiye mshindi wa kwanza wa shindano la golden goal kupitia mchezo wa bahati nasibu wa Betway. Koech mwenye umri wa miaka 27 na anayetoka katika kaunti ya kericho amejishindia safari ya Uingereza kutazama mechi kati ya Arsenal na West Ham uwanjani Upton Park mwezi Aprili. Koech amesema kuwa alijaribu mara kadhaa bila kufanikiwa na ushindi huo utampa fursa ya kutazama wachezaji ambao amezoea kuwaona kwenye runinga.