CORD kupinga mswada wa kubadilisha tarehe ya uchaguzi mkuu mwaka ujao
9th February, 2016
Wajumbe wa mrengo wa CORD wamesema watapinga mswada wa kubadilisha tarehe ya uchaguzi mkuu mwaka ujao. Wajumbe hao mapema leo wamefanya mkutano faraghani katika afisi ya Wiper eneo la Lavington kupanga mikakati ya kukabili makali ya wenzao kutoka Jubilee bungeni. Pia wametaka tume ya uchaguzi IEBC ihakikishe kila kituo cha kupiga kura kimepata vifaa vya kusajili wapiga kura.