Gavana wa Muranga Mwangi wa Iria afika mbele ya tume ya EACC
8th February, 2016
Gavana wa Muranga Mwangi wa Iria amefika mbele ya tume ya maadili na kupambana na ufisadi EACC. Iria anatuhumiwa kuwangaisha maafisa wa tume hiyo waliovamia makao yake wiki mbili zilizopita. Maafisa hao walivamia makao ya gavana Iria huko Thika kwa madai kwamba anahusika katika utumizi mbaya wa mamlaka,ufisadi na mapendeleo katika kutoa zabuni na ununuzi katika kaunti.