Kauli ya wana CORD kuhusu Jaji Tunoi
6th February, 2016
Wanasiasa katika muungano wa cord wametoa kauli mbalimbali kuhusiana na sakata ya rushwa inayohusishwa na jaji wa mahakama ya juu zaidi Phillip Tunoi. Seneta wa Bungoma Moses Wetangula na mbunge wa Kiminini Chris Wamalwa wamesema kuwa watamuunga mkono jaji Tunoi ikiwa watatambua kuwa anasingiziwa. Naye mkurugenzi wa uchaguzi wa ODM ambaye ni mbunge wa suna mashariki Junet Mohamed amesema kuwa hivi karibuni cord itafichua maovu katika idara ya mahakama.