Serikali ya kaunti ya Elgeyo Marakwet kuzindua rasmi mbuga ya wanyama ya Rimoi
2nd February, 2016
Serikali ya kaunti ya Elgeyo Marakwet imetangaza kuzinduliwa rasmi kwa mbuga ya wanyama ya Rimoi. Mbuga hiyo itakayozinduliwa rasmi tarehe 11 mwezi ujao ni moja wapo ya njia za kuwakaribisha watalii katika kaunti hiyo . Gavana wa Elgeyo Alex Tolgos ameitaja kaunti hiyo kuwa yenye raslimali za kutosha kuwavutia watalii wa humu nchini na kimataifa . Tolgos alikuwa akizungumza alipozuru makao makuu ya standard group ambapo amekutana na afisa mkuu mtendaji Sam Shollei .