Wanaharakati wa haki waolaumu serikali ya Jubilee kwa kuendeleza njama za kuiharibu katiba mpya
1st February, 2016
Wanaharakati wa haki na baadhi ya wabunge wa CORD wamesema serikali imekuwa ikiendeleza njama za kuiharibu katiba mpya. Wakizungumza kwenye kikao cha shirika la jamii la K.A.R.A hapa jijini Nairobi wanaharakati John Githongo na mbunge wa Ruaraka Tom Kajwang ambaye pia ni mwanachama wa kamati ya masuala ya haki na sheria bungeni, wamesema serikali imekuwa ikianzisha sheria zinazopunguza makali ya katiba mpya .