Familia za wavulana waliofariki kwenye ajali ya Salgaa bado wanasubiri kutendewa haki
1st February, 2016
Familia za wavulana wa chini ya umri wa miaka 18 waliofariki kwenye ajali ya Salgaa, usiku wa kuamkia mwaka mpya, bado zinasubiri kutendewa haki. Familia hizo zinasema kuwa polisi aliyewakodisha wavulana hao gari yungali huru licha ya kukiri kwamba gari lilikuwa lake.