Mzozo umeibuka kuhusu kufungwa kwa bandari ya Mombasa
29th January, 2016
Biashara ya mabohari ya kuhifadhi bidhaa mbalimbali katika bandari ya Mombasa ni maarufu mno. Hata hivyo serikali katika siku za hivi karibuni imekuwa ikiagiza kufungwa kwa baadhi ya biashara hizo kwa sababu mbalimbali, moja wepo ni kuhakikisha kuwa hazihifadhi bidhaa za magendo. Hata hivyo kufungwa kwa biashara ya kampuni ya auto port freight terminal kumeibua siasa kali.