Uhuru akutana na rais wa Nigeria Muhammadu Buhari
28th January, 2016
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ambaye yumo nchini katika ziara rasmi ya siku tatu alifanya mazungumzo na rais Uhuru Kenyatta katika ikulu ya Nairobi mapema hii leo. Mazungumzo yao ambayo yaliwahusisha maafisa wa serikali hizo mbili yalijikita katika mbinu za kuboresha uhusiano wa kidiplomasia na biashara kati ya Kenya na Nigeria ambayo inatambulika kwa rasilmali kubwa ya mafuta. Vivyo hivyo rais Uhuru Kenyatta aliangazia suala la Kenya na Nigeria kukabili tatizo la ugaidi ambalo limeathiri nchi hizi mbili.