Kashfa ya Eurobond: Kiongozi wa Cord Raila Odinga ampongeza Keriako Tobiko
23rd January, 2016
Kiongozi wa muungano wa CORD Raila Odinga ameipongeza hatua ya mkurugenzi wa mashtaka nchini kenya Keriako Tobiko kuagiza kufunguliwa tena kwa faili zinazoambatana na ile kashfa ya Eurobond ili waliofaidi watajwe. Akizungumza katika kaunti ya Vihiga kwenye hafla ya mazishi, Raila amesema hilo likifanyika litaondoa utata wote unaozingira sakata hiyo. Seneta wa Vihiga George Khaniri, na aliyekuwa spika wa bunge Kenneth Marende ni kati ya waliohudhuria hafla hiyo.