Gavana wa Embu Martin Wambora apiga marufuku kuuzwa kwa kahawa kutoka kaunti hiyo
18th January, 2016
Gavana wa kaunti ya Embu Martin Wambora amepiga marufuku ya kuuzwa kwa buni au ukipenda kahawa ambayo haijatayarishwa nje ya kaunti ya Embu. Hatua amesema inachukuliwa kuwakinga wakulima wa kahawa kaunti ya Embu dhidi ya wanunuzi wanaowapunja pesa zao,kwa kununua buni kwa bei nafuu.