Naibu wa Rais William Ruto ajitetea katika Mahakama ya ICC
14th January, 2016
Ni siku ya tatu katika mahakama ya icc ambapo wakili wa naibu wa rais William Ruto anaendelea kutoa sababu za ni kwanini kesi hizo zinapaswa kutupuliwa mbali. Kareem khan ameulaumu upande wa mashtaka kwa uchunguzi finyu hivyo basi kuacha baadhi ya mambo muhimu licha ya kusisitiza kuwa hata wao wana ufahamu kuwa kesi hiyo haina mwelekeo.