Raila Odinga yaangusha shoka la Eurobond kwa kutaja wahusika wakuu
14th January, 2016
Baada ya ngoja ngoja ya muda hatimaye kiongozi wa cord raila ametoa orodha ya majina ya watu wanane anaodai ni wahusika wakuu kwenye sakata ya eurobond. Waziri wa fedha henry rotich, katibu wa fedha dkt kamau thugge na mwenyekiti wa benki kuu mohammed nyaoga ni miongoni mwa wanane hao.