Familia moja katika eneo la Othaya yapata mwili wa binti yao kwenye kisima
11th January, 2016
Familia moja katika eneo la Othaya imekumbwa na majonzi baada ya kuupata mwili wa binti yao mwenye umri wa miaka 17 kwenye kisima. Mwili huo ulikuwa na majeraha yanayoashiria kwamba huenda alibakwa kabla kuuawa. Nyanyaye binti huyo amesema alimwacha na mjakazi wa nyumbani siku ya jumapili na kwenda kanisani na akirejea hakumwona tena.