Polisi mjini Mombasa wanasa mshukiwa wa ugaidi
5th January, 2016
Polisi mjini Mombasa wanamzuilia mshukiwa mmoja wa ugaidi huku wakiwasaka wengine wanne waliokwepa mtego wa walinda usalama kwenye maficho yao eneo la Majengo. Polisi walipata bunduki mbili zilizoibwa mwaka jana baada ya washukiwa hao kumwua polisi na mwanajeshi.