Mfadhili atoa matiti bandia kuwapa moyo waathiriwa wa saratani ya matiti Kirinyaga
4th January, 2016
Ni dhahiri kuwa mwanamke huthamini matiti yake. Aidha siku hizi inaaminika kwamba viungo hivyo muhimu ndivyo vinavyomtambulisha mwanamke kwenye jinsi ya kike. Kwa hivyo mtu anapojipata akiugua saratani ya titi na kulazimika kufuata ushauri wa daktari wa kukatwa titi hilo au yote mawili, Wengi husikitika..mwanamke mmoja anayeishi barani Ulaya amerejea katika eneo la Kirinyagah na mradi wa kutoa matiti bandia angalau kuwapa moyo waathiriwa wa kensa ya matiti.