Wazazi walalamikia gharama ya masomo ambayo inaendelea kupanda huku shule zifunguliwa
3rd January, 2016
Muhula wa kwanza wa masomo unatarajiwa kuanza hapo kesho huku wazazi wakilalamikia gharama ya masomo ambayo inaendelea kupanda. Mbali na baadhi ya shule kuongeza karo kwa viwango vya juu, gharama ya vitabu pia inawakosesha wazazi usingizi. Lakini wachapishaji vitabu wanailaumu serikali kwa kile wanachokitaja kuwa kuongeza kodi kwa mali ghafi ya kutengeneza vitabu.