Magavana wataka ugatuzi ulindwe na wananchi na serikali
2nd January, 2016
Tunapoanza mwaka wa 2016 leo, huenda ndio mwaka ulio na mtihani mkubwa sana kwa ugatuzi ikizingatiwa kwamba muda wa kuhamisha baadhi ya huduma kutoka serikali kuu kwa serikali za kaunti utakamilika mwezi machi. Akizungumza katika hafla ya kuadimisha mwaka mpya, mwenyekiti wa baraza la magavana peter munya amesema kuwa juhudi za kufanya mabadiliko katika baadhi ya huduma hazijafua dafu.