Mhubiri David Owuor afika Kisumu kwa kishindo kwa maombi iliyowavutia maelfu ya Wakristo
31st December, 2015
Kila mwaka unapofikia kilele wakenya huukaribisha kwa njia mbali mbali. Baadhi hufika katika maeneo ya burudani, wengine kanisani, baadhi wakisalia nyumbani. Lakini mji wa Kisumu umempokea mgeni wa kipekee ambaye ameandaa maombi katika uwanja wa Kibos ambayo yamevutia maelfu ya Wakristo kutoka hapa nchini na nje ya nchi.