Wabunge wa Jubilee waandaa mikutano Pokot Magharibi kuwarai wananchi kuunga chama hicho
28th December, 2015
Wabunge wa Jubilee wameandaa mikutano katika kaunti ya Pokot Magharibi kuwarai wananchi kuunga mkono chama hicho kinachoongozwa na rais Uhuru Kenyatta. Ni mikutano iliyoandaliwa na mbunge wa Pokot kusini David Pkosing, mbunge wa Kacheliba Mark Lomunokol na mbunge wa Webuye Magharibi kwa matayarisho ya uchaguzi wa mwaka 2017.