Watu 2 wauawa na wanajeshi wa KDF mjini Mandera
28th December, 2015
Watu 2 wameuawa na wanajeshi wa KDF mjini Mandera mapema leo asubuhi huku wengine 5 wakipata majeraha ya risasi. Kulingana na maafisa wa KDF,walisikia mlio wa kilipuzi walipokua wakishika doria huku gari aina ya probox likiwapita na kuamua kulifyetulia risasi, kauli ambayo imepingwa vikali na wenyeji pamoja na viongozi wa kaunti ya Mandera. Tukio hilo limeirudisha nyuma imani ya wenyeji na vyombo vya usalama sehemu ya kaskazini mashariki katika vita dhidi ya ugaidi.