Maafisa wawili wa Polisi wauwawa katika shambulizi la Mandera
27th December, 2015
Maafisa wawili wa polisi wameuawa huku wengine wakijeruhiwa waliposhambuliwa na watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa al- shabaab, katika barabara inayoelekea el wak kaunti ya mandera. Shambulizi hili linatukia siku mbili tu baada ya msafara wa maafisa wa polisi kushambuliwa kaskazini mwa kenya na kundi hilo hilo la al shaba ambapo afisa mmoja aliuawa. Tukio hilo limewashinikiza kwa mara nyingine tena viongozi kutoka kaunti ya mandera kukusanyika na kuitaka serikali ya rais uhuru kenyatta,kulishughulikia swala la ukosefu wa usalama wa kutosha sehemu hio.