Mashindano ya Ndondi yaandaliwa katika Kaunti ya Mombasa
26th December, 2015
Huku wengi wakiendelea kujivinjari kwenye siku kuu ya boxing kwa kutoa au kupokea zawadi, wenyeji wa mji wa Mombasa walipata kutumbuizwa na chipukizi kutoka kaunti hiyo kwenye mashindano ya ndondi.mashindano hayo yaliwaleta pamoja vijana kutoka kaunti hiyo kwa ajili ya kuonyesha talanta zao kwenye mchezo huo wa masumbwi. Waandalizi walinuia kutumia mashindano hayo kama njia mojawapo ya kuwasaidia vijana kwenye kaunti hiyo kuepuka utumizi wa madawa ya kulevya. Fainali za mashindano hayo zitaandaliwa siku ya jumatatu.