Sherehe za waturkana yawaleta pamoja familia
24th December, 2015
Ilikua ni furaha na nderemo wakati maelfu ya watu kutoka jamii ya Ateker walipoungana kusheherekea na kumkumbuka mama yao Nayeche katika eneo la Moruanayeche sehemu ya letea kaunti ya Turkana. Jamii za wateso na wakaramojong kutoka Uganda, toposa kutoka Sudan kusini na nyang’atom kutoka Ethiopia waliungana na wenzao waturkana kumkumbuka mama huyo.