Watu wawili wafariki na wengine watatu kujeruhiwa katika shambulizi la Mandera
21st December, 2015
Watu wawili wameuwawa huku wengine zaidi wakiuguza majeraha baada ya kundi la watu kuwashambulia abiria katika basi moja kaunti ya mandera. Lakini katika taswira ya kuonyesha umoja wa jamii ya waislamu waliokuwa katika basi hilo lililokua likitokea mandera kuja hapa mjini nairobi, abiria wa kiislamu waliwazingira wenzao wa kikristo na kuwakinga dhidi ya kuuawa, baada ya kundi la wanamgambo wa al-shabaab kuwatenganisha tayari kuwaua. Mwanahabari mwenzangu hussein mohammed na taarifa hiyo.