Mkutano wa kimataifa WTO wakamilika Nairobi kwa kutoa maazimio yaliyoafikiwa
19th December, 2015
Hatimae mkutano wa kimataifa wa kibiashara wa WTO,umekamilika kwa kutoa maazimio walioafikiana kuhusu sera za biashara. Mapema leo mashirika yasiyo ya serikali yalifanya maandamano nje ya ukumbi wa kicc wakilalamikia kutengwa kwa mataifa yanayokumbwa na umaskini na mataifa yanayozidi kunawiri katika kongamano la kibiashara la WTO. Mashirika hayo yamelaumu mataifa yaliyonawiri kwa ubinafsi yakitaka usawa kuzingatiwa.