Rais mstaafu Daniel Moi aomba serikali kuhakikisha watoto wanapata elimu bora kwenye vyuo
18th December, 2015
Rais mstaafu Daniel Arap Moi ametoa changamoto kwa serikali na wazazi kuhakikisha kwamba watoto wao na kizazi kijacho wanapata elimu bora kwenye vyuo vilivyoidhinishwa ili kuepuka vyuo bandia vinavyochipuka kote nchini. Mzee Moi aliwapa wasia wale waliofuzu wawe wa kurudisha mkono wa shukran katika jamii na kuwa watu wa manufaa kwa wazazi wao. Alizungumza mapema leo alipokuwa akiongoza hafla ya kufuzu ya chuo kikuu cha Kabarak kaunti ya Nakuru. Sherehe hiyo ya 11 tangu chuo hicho kianzishwe, ilifanyika kwenye bewa kuu la chuo hicho huko Nakuru