LIPENI KWANZA: Hospitali katika Kaunti ya Migori yakatalia mwili wa marehemu
6th December, 2015
Familia moja katika kaunti ya migori ambayo huishi maisha ya uchochole inapitia hangaiko la aina yake kupata shilingi milioni moja kulipia ada ya hospitali ili ipewe maiti ya mpendwa wao. Marehemu alikuwa fundi wa nyaya za umeme na alifariki kutokana na majeraha aliyopata baada ya kuanguka kutoka kwenye mlingoti wa umeme akiwa kazini.