Kizaaza chazuka baada ya mwanamke mmoja kujaribu kusimamisha harusi ya aliyekuwa mumewe
5th December, 2015
Wakaazi wa mtaa wa Imara Daima walijionea sinema ya bure mchana pale mama mmoja alipojaribu kusimamisha harusi iliyohusisha anayedai kuwa mumewe na mwanamke mwengine. Anne Nyamweya amedai kuwa mumewe alipanga mipango ya harusi kwa misingi kwamba mkewe alikuwa tayari ameaga dunia na hata kubadilisha vyeti vya kuzaliwa vya wana wao wanne. Kinaya kikuu ni kuwa harusi hiyo iliendelea kama ilivyopangwa licha ya mvutano uliokuwepo. Nick Wambua na taarifa hiyo.