Kutana na Ryan Thuku na Jason Oyuchi, watoto walio na uwezo wa kusoma kama macho yamefungwa
21st November, 2015
Binadamu humiliki vipaji na talanta mbalimbali kama vile uigizaji, uchoraji,uimbaji na kadhalika. Lakini kisa kimoja cha mtoto aliye na uwezo wa kusoma kama macho yamefungwa kinastaajabisha na kuwaacha wengi na maswali chungu nzima. Ryan Thuku aliye na umri wa miaka tisa anakipawa hicho maalum cha kuona kama amefumba macho. Na isitoshe, kakake mdogo Jason Oyuchi pia ana kipawa kama hicho.