Mwanamke afariki kutokana na utepetevu katika hospitali kuu ya Kakamega
16th November, 2015
Kwa mara nyingine tena, hospitali ya rufaa ya Kakamega imejipata pabaya. Kisa na sababu ni kifo cha mwanamke mwingine wiki moja baada ya kujifungua kufuatia utepetevu wa wahudumu wa afya hospitalini. Yadaiwa abigael chesang mwanafunzi wa chuo kikuu cha masinde muliro alifariki baada ya kusubiri kwa muda wa saa 12 bila kuhudumiwa ila alipewa tu dawa za kupunguza maumivu akihudumiwa na wahudumu wasio na ujuzi. Jee madaktari walikuwa wapi? Itakumbukwa mtazamaji ni wiki mbili tu zimepita baada ya hospitali ya kakamega kugonga vichwa vya habari kwa kumtelekeza mwanamke aliyehitaji huduma ya dhahurura ya upasuaji baada ya mtoto wake kufariki tumboni. Mary kilobi anaarifu zaidi.