Viongozi mbalimbali kote duniani watoa rambirambi kwa Ufaransa kutokana na shambulizi la kigaidi
14th November, 2015
Viongozi wa nchi mbalimbali kote duniani wanazidi kutoa risala za rambirambi kwa Ufaransa kutokana na matukio ya kigaidi yaliyowaua zaidi ya watu 120. Kundi la wapiganaji la Islamic State limesema kuwa lilihusika katika mashambulizi hayo yaliyowaacha zaidi ya watu mia mbili wakiwa wamejeruhiwa.