Huduma za hospitali za umma zazidi kuzorota
12th November, 2015
Tunaanza habari zetu leo kwa suala ambalo limeanza kuwatatiza wakenya wanaotafuta huduma katika hospitali za umma. Si mara moja baadhi ya wakenya wamefariki kwa kukosa huduma huku wengine wakiugua zaidi baada ya kuhudumiwa. Leo tunaangazia kisa cha familia moja ambayo sasa inapitia mahangaiko baada ya kumpeleka mtoto wao katika hospitali kuu ya kenyatta kutibiwa lakini akarudi nyumbani akiwa amepoteza uwezo wa kuona.