Shirika la Kandanda nchi awaonya wanariadha dhiidi ya kutumia madawa ya kulevya
31st October, 2015
Afisa mkuu mtendaji wa chama cha riadha nchini Isaac Mwangi ameeleza kuwa mikakati kabambe itawekwa ili kuzuia visa vya utumiaji wa dawa ya kusisimua misuli katika riadha. Mwangi, aliyekuwa akizungumza katika uzinduzi wa mbio za nyika za tuskys wareng aliongeza kuwa wataanzisha shughuli ya kuwafanyia uchunguzi wanariadha katika mashindano yote humu nchini ili kukomesha tatizo hilo ambalo limeugubika ulimwengu wa riadha katika miaka ya hivi karibuni.